Audio ya Sinema ya Yesu Katika Kisukuma
  
Audio ya Sinema ya Yesu Katika Kiswahili

Monday, April 4, 2011

ROSE MUHANDO SAFARINI LOLIONDO ???

Malkia wa muziki wa Injili nchini, Rose Muhando, amedai kupanga safari ya kwenda  kijiji cha Samunge, wilayani Loliondo kukutana na Mchungaji, Ambilikile Mwasapile kwa lengo la kunywa dawa ili siku ya Tamasha la Pasaka linalotarajiwa kufanyika mwezi ujao limkute akiwa fiti.

Rose alitoa kauli hiyo hivi karibuni ndani ya  Studio za Zoom Production, zilizopo Magomeni Usalama jijini Dar es Salaam anakorekodia nyimbo zake kumi kwaajili ya albamu yake ya tatu.

Mkali wa Injili ambaye nyimbo zake huonekana mpya kila kukicha alisema kuwa, baada ya kupata taarifa ya tiba za Babu huyo alikuwa na mashaka nazo lakini kadiri siku zinavyokatika ameanza kuziamini kutokana na ushuhuda za watu mbalimbali wanaohudumiwa.

Endapo Rose atatekeleza adhima yake hiyo, atakuwa mwimbaji wa kwanza wa muziki huo kujitangaza kwenda kupata tiba kwa Babu wa Loliondo ambayo imekuwa ikiwagawa watumishi mbalimbali wa Mungu ambao kila mmoja amekuwa akisema lake.

Chanzo: Blogu ya Kabula George

No comments: