O'LOLO - EMMY KOSGEI

MPINGA KRISTO - KWAYA YA A.I.C CHANG'OMBE

NYIMBO 49 ZILIZOCHAMBULIWA

NISHIKE MKONO - FANUEL SEDEKIA

BIBLIA YASEMA - MCH. ABIUDI MISHOLI NA FARAJA BAND


NYIMBO 142 KUTOKA WAVUTI.COM

MAHANGAIKO - KWAYA YA MUUNGANO MWANZA

FUATILIA NYIMBO ZA DINI HAPA

NYIMBO 158 KUTOKA WAVUTI.COM

SAMEHEANENI - REBECCA MAGABA

Wednesday, November 16, 2011

Habari: Martha Mwaipaja Achumbiwa

Na Gladness Mallya

Mwimbaji wa muziki wa Injili nchini, Martha Esau Mwaipaja (pichani)  amechumbiwa na Mchungaji, John Said anayehudumia Kanisa la Udhihirisho wa Injili lililopo Ukonga jijini Dar es Salaam, Risasi Jumamosi linakupa habari kamili.

Habari zisizo na chenga zilizotua kwenye meza ya gazeti hili juzikati zilisema, Martha atavishwa pete ya uchumba na mchungaji huyo kesho saa 6:00 mchana katika Kanisa la Victoria lililopo Ubungo External jijini Dar.

“Martha anavishwa pete ya uchumba Jumapili (kesho) na Mchungaji, John Said na baada ya zoezi hilo kutakuwa na sherehe ndogo kanisani hapo kwa ajili ya kumpongeza kwa kufikia hatua hiyo,” alisema mtoa habari ambaye hakutaka jina lake lichorwe gazetini.

Alipotafutwa kuzungumuzia suala hilo, Martha alikiri kuchumbiwa na mchungaji huyo na kuongeza shughuli ya kesho itanogeshwa na waimbaji wenzake kama vile Bahati Bukuku, Sarah Mvungi, Ambwene Mwasongwe na Christina Mwang’onda.

Wengine ni David Robert, Debora John, Josephine Mwasulama, Ado November, Jennifer Mgendi, Lianga George, Stella Swai na wengineo.
Chanzo: Risasi (Novemba 12-14)

0 comments:

VITAMBULISHO VYA WATUMISHI WA BWANA