Audio ya Sinema ya Yesu Katika Kisukuma
  
Audio ya Sinema ya Yesu Katika Kiswahili

Saturday, March 7, 2009

MWAMBA - MAXIMUM MELODIES

8 comments:

Anonymous said...

ONDOA HII PICHA KUWA YA KWANZA.HIYOLABEL INA SUGGEST BLOG NI YA KENYA .

Anonymous said...

We Anonymous. Kuna shida gani kusikiliza nyimbo za Kenya? Sielewi tatizo ni nini. Ni wimbo hukuupenda au nyimbo za dini za Kenya ndiyo tatizo. Huo ni wimbo na umetengenezwa na Kenyangospel.com. Tatizo liko wapi? Fafanua please!

Anonymous said...

KAMA WEWE MKENYA SI AJABU HUJANIELEWA.
KAMA NI MBONGO, KENYA WANACLAIM MIZIKI MINGI INATOKA KENYA.

KAMA IDENTITY YA WIMBO HAINA TATIZO ,KWA NINI MPAKA LEO WANASISITIZA WIMBO MALAIKA UMETOKA KENYA?KWANINI WASISEME OK,WIMBO HUU NI WATANZANIA.

SISAHIHI KUWEKA WIMBO WA BURUNDI KISHA UWEKE LABEL YA RWANDA.

UNAWEZA KUWEKA NYIMBO HATA ZA ETHIOPIA,LAKINI BAINISHA NI ZA ETHIOPIA ,USIJARIBU KUZIFANYA ZIONEKANE NI ZA KENYA.

WAPE NAFASI WANAMUZIKI KUWA PROUD NA WALIPOTOKA. LABEL,HAKIMILIKI,UTAIFA,IDENTITY.

Anonymous said...

Anony. hapo juu: Huu wimbo upo katika youtube na link yake hii hapa:

http://www.youtube.com/watch?v=9qHZ2FLgoFU.

Huko utaziona nyimbo zao nyingine. Mimi nadhani wamefanya vizuri kuweka label yao kwani kokote clip hii itakakotazamwa na kusikilizwa basi itajulikana kwamba ni yao na hii ni njia nzuri ya kujitangaza na kujulikana - mbali na kueneza INJILI. Hizo issues zako za utaifa, ukabila, identity n.k. ni za kwako wewe.

UNAWEZA KUWEKA NYIMBO HATA ZA ETHIOPIA,LAKINI BAINISHA NI ZA ETHIOPIA ,USIJARIBU KUZIFANYA ZIONEKANE NI ZA KENYA.

Mimi si Mkenya na ninachofanya hapa ni kukusanya tu nyimbo za dini kutoka you tube na kwingineko BILA KUJALI UTAIFA, UKABILA na kuziweka hapa kama zilivyo. Na karibu kila clip ina jina la wimbo na msanii mwenyewe. Nami ninapoziweka hapa basi naweka jina la wimbo na msanii. Na wakati mwingine hata sijui msanii anatoka nchi au ni wa kabila gani kwani hii haina umuhimu wo wote. Lengo langu ni kuwapa watu access ya nyimbo za dini na hasa za Kiswahili in one place. Mungu akubariki!!!

Anonymous said...

Wewe usiye na jina hapo juu usichanganye watu hapa na mambo yako ya utaifa, ukabila na siasa. Nadhani unahitaji maombi wewe. Kama unataka mjadala wa haya mambo yako ya utaifa na ukabila nenda ukasome makala za Mobhare Matinyi katika IssaMichuzi.blogspot.com na kama unazo points basi ka-argue huko. Hapa si mahali pake na please tuache tupate injili bila kujali UTAIFA. Yesu mwenyewe alisema NENDENI MKAITANGAZE INJILI KATIKA MATAIFA YOTE...Hakusema mkifika Kenya fanyeni hivi, mkifika Tanzania fanyeni hivi...Ubarikiwe!

Anonymous said...

Maombi ? ya nahitaji maombi, mimi sio mtakatifu kama wewe.

Mi blog sio yangu, lakini blog yako haina kitu chochote kinacho onyesha utaifa.
Kama kuonyesha utaifa ni kosa kwa nini hawa wakenya nyimbo hawaziachi blank au waweke label Tanzania.
Kutokuwa tayari kukabiliana na dunia ya sasa ndiyo inayo tufanya tuchelee kukubali jumuia huru EA. .. hata wanyawanda watatupiga bao.
Yesu alikuja kwa mataifa yote ?

fs said...

nina watakia siku kuu njema amen

fs said...

na nyimbo yenu mwamba na ipenda sana na tena sana.
uyu ni FRANCOIS BARAGORA.