Audio ya Sinema ya Yesu Katika Kisukuma
  
Audio ya Sinema ya Yesu Katika Kiswahili

Tuesday, May 26, 2009

ETI, KUPIGA NYIMBO ZA INJILI KATIKA MABAA NI SAWA?

8 comments:

Anonymous said...

Acheni injili ya Mungu ihubiriwe popote pale. Kutakuwa na sherehe na vifijo mbinguni kama mlevi mmoja ataokolewa. Mimi nadhani ni sawa tu kupiga nyimbo za dini kwenye mabaa. Huwezi jua mipango ya Mungu.....

Mbele said...

Mimi ni Mkristu. Sielewi kwa nini nyimbo za dini yetu zinapigwa kwenye baa. Wakristu tukiendekeza tabia hii ya kutopambanua masuala ya ibada na masuala ya ulabu, mwishoni tutakuwa tunatwanga bia kanisani.

Kuna masuala mengine ambayo yanaonyesha kuwa Wakristu tumepotea njia. Vitabu vyetu vitakatifu, kama Biblia, utavikuta vimezagaa hata gesti, katikati ya vyupa vya bia na konyagi na vitu vingine visivyotajika. Muislam namheshimu, kwani anaheshimu vitabu vya dini yake. Hutavikuta vimezagaa namna hiyo.

Hata hizo nyimbo za dini zinazotamba baa ni za dini yetu Wakristu. Sijamwona Muislamu akidhalilishi nyimbo za dini yake namna hii.

Anonymous said...

Mimi nadhani nitasilimu tu na kuwa Mwisilamu. Ninaamini kwamba Biblia yetu imechafaliwa sana kwa kutafsriwa hovyo hovyo. Leo hii Ukristo umegeuzwa biashara. Tazama akina Kakobe walivyojitajirisha kwa kutumia fungu la 10 kutoka kwa waumini waliokuwa "indocrinated" Inasikitisha sana! Biblia, nyimbo na kila kitu cha Kikristo unaweza kukifanya cho chote unachotaka. Hebu iguse Korani uone moto utakavyokuwakia!

Laiser said...

Wapendwa, kuna mambo mengi ambayo yatakiwa kufanyiwa marekebisho, hasa kwa habari ya Ukristo. Tunasahau jina tulilonalo la kuitwa "Mkristo" kuwa ni jina la ajabu. Jambo lingine mara nyingi tumesahau habari ya Mungu wetu kuwa "Roho" nao wamwabuduo inawalazimu kumwabudu katika Roho.
Nadhani tukiyafahamu yayo, na kusudi letu kama Wakristo, nadhani tutaweza kuyatenda yatupasayo.
Mungu atusaidie wote tujue tu viungo katika mwili wa Kristo, zaidi sana kazi ya kila kiungo katika kuikamilisha.

Mzee wa Changamoto said...

Mmmmh! Mjadala mkubwa na mzuri huu. Kama nilivyowahi kusema, kuna mengine ya kujiuliza kuhusu maisha yetu. Bado nahisi kuna ukweli katika hili lililosemwa japo naamini kuna wanaolikuza kuliko lilivyo. Nimekuwa na mijadala kadhaa kule Strictly Gospel kuhusu hili na mengine mengi. Tatizo linakuja pale ambapo wenye kuonekana wanatetea, wanakuja na references ambazo zinaonesha mapungufu mengi ya uelewa wa Neno la Mungu. Lakini nami niliwahi kuuliza matumizi ya NENO LA MUNGU kwa dini zote kwa namna linavyotumiwa na viongozi mbalimbali. Bofya hapa http://changamotoyetu.blogspot.com/2009/01/hivi-marais-wana-dini-ama-imani.html kusaidia kuona kama tunatenda tusemalo ama tunasema kwa kuwa ni utaratibu na kutenda kwa kuwa sehemu ya maisha inatulazimisha kutenda hivyo. Wanaopiga nyimbo za injili, ni kwa kuwa zinaleta wateja, japo wanajua kuwa haziendani na "biashara" zao. Lakini unapokosa muungano wa Imani yako na Maisha yako ya nje, maisha hayatakuwa sawasawa.

Mzee wa Changamoto said...

Sasa na huyu Injilia kalitumiaje neno la Mungu? http://issamichuzi.blogspot.com/2009/06/aua-wawili-na-kujeruhi-saba-kwenye.html#comments

Anonymous said...

Ni sawa, Yesu hakuja kwa watu safi, bali waliopotea. Mtu mzima haitaji tabibu...

Waache wapate neno la Mungu hukohuko baa. Kila mtu alisikie neno kabla huo mwisho haujaja....
Ni hayo tuuuuuu

Anonymous said...

mtoa maoni anayesema utasirimu mimi nakushauri kuwa kubadili dini sio suluhisho kwani huko nako kuna matatizo makubwa inawezekana zaidi ya hayo mfano watu kujitoa muhanga na kuuwa watu wasio na hatia au kuwapiga wanawake wazinzi mawe hadi wanafariki dunia hivyo kabla hujafanya jambo jaribu kufikiria mara mbili mbili