Audio ya Sinema ya Yesu Katika Kisukuma
  
Audio ya Sinema ya Yesu Katika Kiswahili

Friday, October 30, 2009

UJUMBE HUO KUTOKA KENYA

3 comments:

Mama Jane (Kariakoo) said...

Hawa wanadanganyana kwamba mwisho wa dunia ni Julai 18, 2010. Yesu ni kweli anakuja lakini hakuna aijuaye saa wala nyakati, HATA MWANA bali BABA PEKEE. Wengi walijaribu kutabiri wakashindwa - na huu hasa ndiyo mwanzo wa kanisa la Wasabato. Kuweni na wasiwasi na mtu/kikundi cha watu/au dhehebu linalojaribu kupanga siku ambapo dunia hii itafikia kikomo/kurudi kwa Yesu. Hakuna ajuaye na tunachoweza kufanya ni kujiweka tayari basi!

MBOGELA, Jackson said...

Nakubalina na wewe mama Jane, lakini shida yangu ni moja watu wengi wamechukua kisingizio cha kusema hatutajua siku wala saa ya kurudi kwa mwana wa adamu kama tiketi ya kula raha za dunia, lakini alishtuonya kuwa "keshini maana yuaja kama Mwivi" kwa hiyo iwe mwakani au mwaka huu au miaka 1000 ijayo tunatakiwa kukesha kila siku, kila wakati

Unknown said...

Ni vizuri kutoa maoni lakini hata Yesu alipodaiwa kutoa ishara alichukia na kukemea"Kizazi cha nyoka mwataka ishara" Kasome Biblia yako. Hakuna aijuaye siku wala saa. Hivi mnakumbuka mtafaruku wa Y2K? Kwamba ifikapo tarehe 1.1.2000 ndo mwisho wa dunia na kompyuta zote zitazimika? Jamani hebu tudumu katika imani Kristo yuaja ila hakuna ajuaye ni lini.