Audio ya Sinema ya Yesu Katika Kisukuma
  
Audio ya Sinema ya Yesu Katika Kiswahili

Friday, November 13, 2009

MKUSANYIKO WA NYIMBO ZA KABULA GEORGE

  • Tembelea blogu za Kabula George na mumewe George Kayala hapa na hapa.
  • Kwa habari zingine kuhusu Kabula George bofya hapa.
(1) DHIHIRISHA


(2) HAKUNA MUWEZA


(3) TUNAISHI KWA NEEMA

2 comments:

Anonymous said...

Hiyo habari kutoka ya Global Publishers itoe ni udaku tu. Huyu mume wake ndiye Mhariri Msaidizi wa Gazeti la Udaku la Risasi - gazeti ambalo linatesa watu kwa kuwazushia mambo ya uwongo. Leo wako hapa eti wanajifanya walokole. Hakuna lolote, kila kitu ni pesa tu. Utakuwaje kwenye gazeti linaloendeleza tabia mbovu, umalaya na ukahaba halafu eti ujifanye umeokoka? Itoe hiyo link ya Global Publishers kwani ni kampeni za kishetani. Usipoitoa mimi sitatembelea blogu hii tena! Mungu akubariki

Limbe Juma said...

Kwa kawaida huwa sijishughulishi sana na comments za ma-anonymous lakini leo nitasema tu kidogo. Kwani kuwa Mhariri wa Gazeti la Udaku ni kosa/dhambi? Hebu basi tusiwe wepesi wa kuhukumu ili nasi tusije tukahukumiwa. Kazi ya kweli ya Mungu inajipambanua yenyewe na kama huduma ya wapendwa hawa siyo kazi yake itajipambanua yenyewe. Sisi ni nani mpaka tuhukumu? Nyimbo za binti huyu wa Mungu ni nzuri, zilizobarikiwa na ukizisikiliza ukiwa umeufungua moyo wako utamwona Roho Mtakatifu Akizungumza nawe. Hebu sote na tukawe na subira na Mungu akaendelee kutubariki daima. Tuombeane, tukishauriana na kutiana moyo kwani safari yetu ni ngumu. Tukianza kukwazana sisi kwa sisi, kweli tutafika?