Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Lengo kuu la blogu ya nyimbozadini ni kuzikusanya video na audio mbalimbali za nyimbo za dini na kuziweka pamoja. Tunatumaini kwamba hii itawapunguzia shida ya kuhangaika kwenda katika mitandao mbalimbali kusaka video na audio hizi. Kwa hivyo video na nyimbo zote zilizopo hapa zinapatikana mtandaoni katika tovuti mbalimbali kama Youtube.com na Google videos. Nyimbozadini.Blogspot.Com haitunzi wala kuuza nyimbo zo zote na kama unataka kununua video za nyimbo utakazoziona hapa basi wasiliana na watoaji au wamiliki wa video hizo. Karibuni tuburudishe mioyo, roho na fikra zetu kwa nyimbo motomoto za Injili. Mungu Atubariki sana!!!
5 comments:
Mbona huu wimbo mmeibabilisha sura yako haionekani na wale dada ulioimba nawe kwani huu sio halisia isipokuwa umefanyiwa decoration.Mdau kinambeu The Hague The Nertherlands
Wimbo asilia ulikuwa na mahadhi ya kiafrika sasa naona mmeona wazungu ni wa maana kuliko waafrika.Napenda nijue ni wewe umebadilisha au ni wezi wa miziki wamefanya mambo yao.Mdau kinambeu The Hague The Nertherlands
Mdau Kinambeu wa The Hague;
Siye mimi niliyeubadilisha kwani siyo mtaalamu hivyo wa kuweza kuedit video nzima na kubadili mandhari nzima. Mimi nimeutafuta mtandaoni na nikaukuta uko hivi hivi na wala hata hiyo mandhari yake ya awali siijui. Nikiupata katika mandhari yake ya mwanzo basi nitautundike upya. Asante sana kwa kuacha maoni yako mara kwa mara na Mungu akubariki sana!
ASANTESANA MASANGU MATONDO NZUZULLIMA KWAJIBULAKO LENYE FARAJA
KWAWASIKILIZAJI WAKIPINDI HIKI.
MUNGU AKUBARIKI ILI UWEZE KUTATUWA
TATIZOHILO HARAKA KAMA ULIVYO AHIDI
Hizi nyimbo bwana...ah, hata sijui niemeje. Kwanza, kama alivyosema anony hapo juu, zimebandikwa mapicha mengine! Sio zile za Beatrice na kikundi chake. Halafuu, kingine kilichoni disappont hapo ni kwamba, sauti ni ya Upendo Kilahiro (hata ilipotoka audi kwa mara ya kwanza walionekana wote -Bitty na Upendo). Then nadhani ukatokea "mtafaruku". Bitty akaziwahi, akazitoa kuwa "ni zake!" Duh! Sauti iliyo solo katika nyimbo karibu zote tunaifahamu, ni ya Mrs Kilahiro bwana!!! (Anyway, hayo ni yao, sie kwakweli tunaburudika na kububujika sana) Barikiweni wapendwa!!!!
Post a Comment